Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda, amebainisha kuwa baba yake
ni moja kati askari kutoka Tanzania ambao wamepigana vita nyingi
kwaajili ya kutetea taifa ikiwemo vita ya kagera mwaka 1978.
Mh. Paul Makonda amesema hayo leo Mei 17, 2018 wakati wa alipokuwa
anatoa salamu kwa Rais Magufuli katika sherehe za ufunguzi wa kituo cha
uwekezaji cha SUMA JKT Mgulani Jijini Dar es salaam na kuongeza kuwa
alizaliwa na kulelewa katika kambi za jeshi
“Nikunong’oneze mheshimiwa Rais, mimi nimezaliwa kambini na baba yangu
ni miongoni mwa askari waliopigana vita nyingi ikiwemo vita ya Uganda na
mpaka ulemavu wake wa mguu ni kutokana na kazi ya kuipigania Tanzania”
amesema Makonda
Makonda aliongeza kuwa kutokana na kulelewa katika kambi za jeshi
imemsaidia kupata ujasiri wa kuongoza mkoa wa Dar es salaam wenye
changamoto nyingi na kuweza kufanya kuwa Jiji la raha Tanzania.
Katika tukio hilo, Rais Dkt Magufuli alizindua kituo cha uwekezaji cha
SUMA-JKT ambacho ndani yake kuna kiwanda cha Ushonaji, Maji, Chuo cha
Ufundi Stadi na Ukumbi wa Mikutano.
Thursday, May 17, 2018
"Baba yangu Alipigana vita ya Kagera" - Makonda
Related Posts:
Makamu wa Rais Samia Aviagiza viwanda Vyote nchini Kutumia Msibomilia (BARCODES) TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania SAMIA SULUHU HASSAN ameviagiza viwanda vyote nchini kutumia msibomilia (BARCODES) za Tanzania kama hatua ya kuimarisha masoko na … Read More
Makonda Apiga Marufuku Kuvuta Sigara Hadharani......Pia Kapiga Marufuku Kuvuta Shisha Baada ya kutangaza vita dhidi ya mashoga juzi, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda jana alitangaza vita nyingine; hataki uvutaji shisha akisema inachanganywa na vilevi vinavyoharibu vijana. Makonda, amba… Read More
CHADEMA Waapa Kutibua Mkutano wa CCM .....Vijana 2000 Kupelekwa Dodoma Kwa Ajili ya Kazi Hiyo CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimepanga kulisaidia Jeshi la Polisi kuzuia Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM). Hivi karibuni Jeshi la Polisi lilitoa zuio la mikutano ya siasa ya wazi na ya ndani … Read More
Rais Magufuli Atuma salamu za Rambirambi Ajali Morogoro Iliyoua Watu 12 TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amezitumia salamu za pole familia, ndugu, jamaa na marafiki wa watu 12 waliopoteza maisha kufuatia ajali mbili zili… Read More
Wabunge Wataka CUF Ifutiwe Usajili Mbunge wa Viti Maalumu, Munira Mustafa Khatibu (CCM) ameiomba serikali kukifuta Chama cha Wananchi (CUF) kutokana na kuhusika na vurugu Pemba. Akijibu swali la Munira kuhusu kufuta chama cha CUF kwa madai kuwa kinac… Read More
TANGAZA HAPA KWA BEI NAFUU
0 comments:
Post a Comment