test

Monday, February 13, 2023

TAMASHA LA LADY IN RED YAFANYIKA JIJINI DAR

 

TAMASHA la ''Lady in Red'' lafanyika Dar wabunifu na wanamitindo chipukizi wapatiwa tuzo kama pongezi ya Sekta ya ubunifu na wanamitindo kutambua mchango wao.

Mkurugenzi wa Kampuni ya Hugo Domingo, Mario Frenandes akizungumza wakati wa tamasha hilo amesema kuwa waandaji wa onyesho hilo kwa Msimu wa pili  wa "Lady in Red limekuwa moja ya jukwaa linalotoa fursa mbalimbali sekta ya ubunifu,wanamitindo, mapambano na Muziki.

"Huu ni msimu wa pili tunaendelea kuunga mkono jukwaa hili lengo ni kuwapa nafasi wenye vipaji kuonekana katika sekta mbalimbali na ndio hasa lengo la Hugo Domingo kuona vijana wanafanya kazi kutokana na ujuzi wao na hata kwenye Tamasha hili hatukubagua tumeshirikiana nao wanamuziki,washereheshaji na wasanii.

Fernandes amesema Tamasha hilo kwa mwakani wanatarajia kufalifanya kwa ukubwa sana na kushirikisha wabunifu kutoka nje huku Tamasha likitarajiwa kufanyika Visiwani zanzibar.

Ameeleza namna jukwaa hilo kwa mwaka huu kutimiza kwake miaka 20 tangu kuasisiwa na Mbunifu Mkongwe Mama Asia Khamsin imepelekea wao kama waandaaji wa jukwaa hilo kwa utofauti na kwa ukubwa zaidi .

"Mitindo sasa hivi inafanya vizuri mwakani tuna mpango wa kuanza visiwani Zanzibar na kilele chake kumalizika Dar es Salaam, hivyo wabunifu wajiandae kuonyesha mavazi yenye viwango vya juu zaidi."
Pia ameongeza kuwa wadau mbalimbali wa sekta ya Mitindo wa endelee kuunga mkono Tamasha hilo ili liendelee kuwepo kila mwaka kwa lengo la kuwaunga mkono wabunifu chipukizi pamoja na wanamitindo.

Katika Tamasha hilo liliweza kutoa tuzo ya Heshima kwa Muasisi wa tamasha hilo Mama Asia Khamsin kwa kutoa vipaji vingi ambavyo kwa sasa ni wabunifu wakubwa Afrika akiwemo Ally Remtullah,Noel stylish pamoja na wengine mbalimbali.

Tamasha hilo ni miaka 20, onyesho la mitindo la Lady In Red limetumika kama jukwaa la kizazi kipya cha mitindo, Lady in Red imeanzishwa na Asya Idarous Khamsin mnamo mwaka 2003.

 Maonyesho hayo pia limewakuza wabunifu wa mitindo mbalimbali  kama vile  Ally Rhemtula, Miriam Odemba, Khadija Mwanamboka, Mustafa Hassanali, Martin Kadinda, Flaviana Matata, Ria Fernandes, Victoria Martin na wengine wengi. 
 
Miaka ya hivi karibuni Asya Idarous alianzisha ushirikiano na kampuni ya Hugo Domingo Limited, kampuni maarufu ya upambaji yenye makao yake makuu jijini Dar es salaam ikiwa na Ofisi pia Arusha, Dodoma, Mwanza, Zanzibar na ikiwa na Mahusiano pia na nchi mbalimbali za Afrika.







Saturday, March 30, 2019

JIFUNZE ZAO LA MAPARACHICHI


Tunda hili lina faida nyingi sana, mbali ya kutumika kama zao la kiuchumi lakini pia hutumika kuimarisha afya ya mwili

1. Faida za Parachichi upande wa Lishe

-Tunda lina vitamini zifuatazo

1. Lina Vitamini A-husaidia sana kuimarisha Macho kuona vizuri

2. Lina Vitamini B (B1-B12)- Husaidia sana mfumo wa misuli ya mwili kuwa sawasa na kuuepusha mwili na matatizo ya nerve

3. Lina Vitamini C-Husaidia sana upande wa kuimarisha ngozi, kwa sababu liko na mafuta, lina zaidi ya mara 4 ya virutubisho vya vitamini C vinavyopatikana katika machungwa

4. Lina vitamini D-ambapo husaidia sana kuimarisha mifupa ya mwili

5. Lina vitamini E-hii husaidia sana kuimarisha seli za uzazi, linasaidia sana kuongeza nguvu na utengenezwaji wa seli za uzazi

6. Lina vitamini K-Husaidia sana kuganda kwa damu, na kuongeza uzalishaji wa chembe hai nyekundu za damu

Madini- (Mineral Elements)
Ni tunda lenye

1. Madini ya Chuma kwa wingi (Fe)-Haya huaidia sana utengenezwaji wa damu, na kuongeza uwezekano wa damu kuwa na oxygeni ya kutosha na kusafirishwa kwa urahisi

2. Madini ya Calcium-Lina madini ya calcium, yanayosaidia kama ufanyaji wa kazi wa seli hai za mwili

3. Lina virutubisho vingine vidogo vidogo vingi, vinavyotakiwa katika ufanyaji kazi mzuri wa selli hai za mwili


2. Agronomy ya ParachichiHali ya hewa

-Ni tunda linalopenda sana sehemu za baridi, maeneo kama ya Rungwe-Mbeya, Njombe, Makete, linastawi vizuri sana, na huwa na Fatty Contenty kubwa

Joto

Nyuzi 15-25 Sentigrade

Muinuko
Mita 1200-1800 kutoka usawa wa baridi

Udongo
-Uwe kichanga tifutifu (Sandy loam), usiotuamisha maji

Aina za Parachichi
1. Zipo aina za kiasiliKila sehemu kuna iana za parachichi ambazo ni za asili ya eneo husika, parchichi hizi, huwa ndefu sana, na mavuno machache

2. Zipo aina za kisasa (Chotara)
Ziko aina nyingi sana za Parachichi chotara, na hizi hapa chini ni baadhi ya zile maarufu hapa tanzania

i. Hass
-Hii ni aina maarufu sana katika aina za parachichi



-Ni tunda linalokuwa na vipere vipere
-Limechongoka juu na chini
-Linahifadhika kwa urahisi

ii. Aina ya pili ni Fuerte
-Hili ni aina ya parachichi lenye ngozi laini saini, ngozi yake inateleza kama imepakwa mafuta
-liko na mafuta mengi ila linawahi kuoza
-Ni zuri kwa matumizi ya kawaida , si kwa kusafirisha umbali mrefu





-Aina hii ikilimwa sehemu za miinuko na baridi sana, inafaa sana kutoa mafuta mengi yanayoweza kutumika kutengeza lotion na baadhi ya vyakula vya mifugo

iii. Aina ya tatu maarufu hapa tanzania -inaitwa X-ikulu
-Ana hii ni maarufu sana kwa mikoa ya nyanda za juu kusini (Mikoa ya Njombe, Iringa, Mbeya na Ruvuma)
-Mti wa aina hii huwa na majani mapana kama mti wa embe
-Mti huu huchukua muda mrefu sana kustawi
-Tunda lake huwa ni kubwa, na lina gharama sana

UPandaji wa Parachichi

Nafasi kati ya shimo na shimo

-Umbali wa kutoka shimo hadi shimo ni MITA 7
-UMbali wa kutoka mstari hadi mstari ni MITA 7

Lakini kipimo hicho hapo juu kitategemea sana na aina ya udongo wa shamba lako , kwa udongo wenye Phosphorus kwa wingi (P), kipimo hicho hakifai, maana baada ya mika 3-5 miche ya mistari miwili inayofuatana itakuwa imekuatana katikati

-Hivyo nafasi yaweza kuwa

8M X 8M-KWA NAFASI HII UTAKUWA NA MICHE 63 KWA EKA 1
AU 9M X 9M-KWA NAFASI HII UTAKUWA NA MICHE 49 KWA EKA 1
AU 10M X 10M- KWA NAFASI HII UTAKUWA NA MICHE 40 KWA EKA 1

Ukubwa wa shimo-Shimo laweza kuwa futi 2.5 x futi2.5 x futi 2.5 = (sm 75 x sm 75 x sm 75) (Kimo x upana x urefu)

-Au kipimo cha futi 3 x futi 3 x futi 3= sm 90 x sm 90 x sm 90

Mbolea

-Mbolea za kupandia zitakazohitajika , ni moja wapo kati ya hizi
-Samadi, Mboji, DAP, au TSP-Lakini ni muhimu kupandia mbolea asilia kama samadi ukachanganya kidogo na TSP au DAP

Kipimo cha mbolea,
-Kama ni mbolea za asili (Samadi au Mboji)-Kiasi cha kilo 16 hadi 20 kinapaswa kiwekwe katika shimo miezi 3 kabla ya kupanda mche

-Kama utapandia mbolea za viwandani (TSP, DAP, Minjingu, NPK etc)
kiasi cha gramu 100 hadi 200 kiwekwe kwa kila shimo, ichanganywe vizuri na udongo, kisha mmea uwekwe na kumwagiliwa

KUKOMAA NA KUTOA MAVUNO
-Parachichi hasa hizi za kisasa, hukomaa baada ya miezi 18 hadi 24

MAVUNO
-Kwa mara ya kwanza mti mmoja wa parachichi unaweza kukupa kati ya matunda 50 hadi 100 kwa mche mmoja.
-Mavuno hueongezeka kadri umri unavyoongezeka
-Mti wa parachichi ukifikia umri wa miaka 4 hadi 5, unakuwa full maturity, na hivyo mti mmoja unaweza kukupa hadi matunda 1200 kwa mwaka mzima '

FAIDA
kwa kipimo cha mita 10 x mita 10, katika eka mmoja utakuwa na mita 40
-Kila mti baada ya mika 5 unaweza kukupa wastani wa matunda 1000
-Hivyo kwa miti 40, utakuw na jumla ya matunda 40 x 1000= 40,000
-Kila tunda kwa bei ya shambani uuze tsh 250, na unamatunda 40,000
-Hivyo utapata jumla ya tsh 250 x matunda 40,000= 10,000,000tsh (MILIONI 10)

Magonjwa ya parachichi

Parcahichi kama mimea mingine inashambuliwa sana hasa upande wa majani pamoja na matunda
1. Yapo magonjwa ya majani, yanayosababishwa na fangasi/Ukungu, Algae, pamoja na wadudu, pamoja na lishe duni
Jani lililoshambuliwa na Alga


Mite-Utitiri mweupe Avocado lililoshambuliwa na Utitiri

2.Magonjwa ya matunda
Yasababishwayo na fangasi/Ukungu, Wadudu,na Lishe dunipia
-Tatizo la Athracnose husababishwa na Ukungu/Fangasi

-Tatizo la Scab, husababishwa na Ukungu/Fangasi hasa wakati wa baridi/unyevu mwingi

 
Thrips wa avocado Matunda yaliyoathiriwa na Thrips


DAWA
-Dawa za kutibu wadudu kama Karate, Matchi, Actellic 50 EC, za faa sana kumaliza wadudu katika mmea wa parachichi

-Dawa za Ukungu kama Ridomil Gold, Ebony 72 WP (Mancozeb na Metalaxyn), Ivory, na Nordox zaweza kutumika kumaliza matatizo ya ukungu

-Lishe ya mmea

Mbolea za kukuzia kama CAN, UREA NA SA (hasa kwenye maeneo yenye magadi kwa wingi, na chumvi nyingi) yaweza kutumika kubalane PH YA Udongo.

-Booster=Mbolea za majani, maua na matunda kama vile Polyfeed Starter, Polyfeed finisher, Wauxal macro mix, Potphos, au Multi K , Ni muhimu sana zikatumika wakati wa maua, na matunda ili kuzuia matunda ya parachichi kuabort (Fruit abortion) yakiwa machanga, pamoja na kuzuia matunda kudondoka yakiwa machanga.


Hitimisho
Parachichi-Kama matunda mengine, ukililima kitaalamu, na ukaweka juhudi na maarifa linakutoa katika umaskini

Monday, May 28, 2018

Rais Na Mwenyekiti Wa CCM Dr Magufuli Aongonza Mkutano Wa Halmashauri Kuu Ya Taifa (NEC) Ya CCM Jijini Dar Es Salaam Leo

Rais wa  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM Dkt. John Pombe Magufuli  akiwa meza kuu katika Ukumbi wa mikutano wa Kikwete katika Mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) wa Chama cha Mapinduzi (CCM) ukumbi wa Kikwete leo Jumatatu Mei 28, 2018  

Katibu Mkuu wa CCM Ndg. Abdulrahman Kinana wakati akisoma muhtasari wa Mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Katika ukumbi wa Kikwete jijini Dar es salaam leo Jumatatu Mei 28, 2018
Wajumbe wakishangilia baada ya  Rais wa  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM Dkt. John Pombe Magufuli kuwaita  Ndg. Mizengo Pinda na Ndg. Makongoro Nyerere waingie ukumbini baada ya kukubaliwa kuwa wajumbe wa Mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) wa Chama cha Mapinduzi (CCM) katika ukumbi wa Kikwete jijini Dar es salaam leo Jumatatu Mei 28, 2018

Uwoya Aelezea Jinsi Mwezi Mtukufu Unavyodumisha Penzi Lake na Dogo Janja

Mwanadada Irene Uwoya na mume wake Dogo Janja amabao kila siku hawaishiwi na drama katika  mitandao wanakuja tena kivingine na kuelezea jinsi mwezi mtukufu wa Ramadhani unavyodumisha mahusiano katika ndoa yao.

Irene anasema kuwa akiwa kama mke halali wa Abdul (janjaro) anahaki zote za kukaa na kutulia kipindi hiki cha ramadhan na kumpikia mume wake  kwa sababu hicho ni kitu alichozoea hata katika ndoa yake iliyopita.
 
"Kuhusu kufunga kwa upande wangu nilishazoea kwa sababu hata siku za nyuma za ramadhani nilikuwa nikifanya hivyo hivyo nilipokuwa na Ndiku na kwa sababu sasa hiv mimi ni mke halali kabisa wa Abdul basi nina haki ya kutulia na kumpikia mume wangu futari."-Uwoya

Vilio Vyatawala Bungeni....Bunge Laahirishwa Hadi Kesho

Naibu Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson leo asubuhi ameahirisha Bunge mpaka kesho saa tatu asubuhi kupisha maombolezo ya kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Buyungu Mwl. Kasuku Bilago aliyefariki siku ya Jumamosi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.
 Vilio na simanzi vilitawala katika ukumbi wa Bunge kutokana na kifo hicho cha Mbunge huyo wa Chadema aliyefariki dunia Jumamosi Mei 26. 

“Waheshimiwa wabunge, Spika wa Bunge mheshimiwa Job Ndugai  anasikitika kuwatangazia kifo cha mbunge wa Buyungu, Kasuku Bilago kilichotokea juzi katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, kwa mujibu wa kanuni zetu, leo shughuli za Bunge hazita endelea na badala yake tutakuwa na maombolezo,” amesema Naibu Spika.

Wakati Naibu Spika Ackson akitoa taarifa za msiba na kuahirisha Bunge, wabunge Julius Kalanga (Monduli), Suzan Kiwanga (Mlimba), Halima Mdee (Kawe) na Dk Semesi Sware (Viti Maalum ) wote wa Chadema walikuwa wakilia.

Mbunge wa Bunda, Ester Bulaya (Chadema) alishindwa kabisa kujizuia na wabunge walilazimika kumpa usaidizi.

Naibu Spika Dkt. Tulia amesema kuwa Wabunge watakao kwenda kuwakilisha kwenye mazishi hayo wataondoka Dodoma siku ya Jumanne asubuhi na kurejea Dodoma Jumatano mara baada ya mazishi hayo kumalizika.

Pamoja na hayo, Naibu Spika ameendelea kwa kusema "siku ya kesho tutakuwa na kikao cha Bunge kama kawaida isipokuwa tutahairisha Bunge saa sita mchana ili kutoa fursa kwa shughuli za heshima za mwisho kwa mwili wa marehumu Bilago na baada ya hapo tutaendelea na maombelezo hadi siku ya Jumatano".

ACT Wazalendo Wahoji Matumizi Fedha Za Korosho

Chama cha ACT Wazalendo kimeitaka Serikali kupeleka haraka asilimia 65 ya fedha za mauzo ya nje ya korosho ghafi kwa Bodi ya Korosho ili zitumike kama zilivyokusudiwa.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mawasiliano ya Umma wa chama hicho, Ado Shaibu, alisema kutokupeleka fedha hizo kutasababisha gharama za uzalishaji kwa wakulima kuongezeka kutokana na ununuaji wa pembejeo kutegemea kwa asilimia 100 katika fedha hizo.

Alisema jambo hilo lilitokea mwaka jana kupanda kwa dawa aina ya salfa (Sulphur) katika maeneo mengi kutoka Sh 16,000 hadi kufika Sh 70,000.

“Kwa mujibu wa sheria ya korosho namba 18 ya mwaka 2009 kifungu 17(A), inaitaka Serikali kuingiza fedha hizo Bodi ya Korosho lakini fedha hizo hazijapelekwa kwa miaka miwili sasa,” alisema Shaibu.

Alisema hata hivyo kwa mujibu wa taarifa ya Bodi ya Korosho iliyotolewa na kamati ya Bunge ya Maji, Kilimo na Mifugo kwa misimu miwili ya mauzo ya korosho, bodi haijapokea fedha hizo na hivyo kuleta athari mbalimbali katika kilimo hicho.

Aliongeza kuwa taarifa hiyo inadai kuwa Bodi ya Korosho haijapokea Sh bilioni 211 ambapo kwa mwaka wa fedha wa 2016/17 wanadai Sh bilioni 91 na 2017/18 wanadai Sh bilioni 110.

“Kutopeleka fedha hizi kutaathiri Kituo cha Utafiti cha Naliendele kinachozalisha mbegu bora za korosho na dawa za kudhibiti magonjwa ambacho kinategemea fedha hizo kwa asilimia 90 kujiendesha kitashindwa kufanya kazi zake kwa ufanisi,” alisema Shaibu.

Aliongeza kuwa athari nyingine ni kuvurugika kwa mfumo wa stakabadhi ghalani kwa sababu ya usimamizi wa mfuko huo kutegemea fedha hizo kwa asilimia 100.

“Mafunzo ya kilimo bora kwa wakulima na maofisa ugani yamesimama kwa sasa kutokana na kukosekana kwa fedha hizo,” alisema Shaibu.

Alisema wanamwomba Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, kulitolea ufafanuzi suala hili ili kuondoa mkanganyiko unaojitokeza.

Akizungumzia kuhusu uchaguzi wa ndani ya chama hicho, Shaibu, alisema umefikia hatua ya majimbo na kitaifa utafanyika Agosti 25 hadi 27, mwaka huu jijini Mbeya.

Alisema chama hicho kinapinga kauli ya Waziri wa Mambo ya Nje, Balozi Augustine Mahiga, aliyoitoa hivi karibuni bungeni kuwa suala la uanachama wa Sahara Magharibi lina utata wa kisheria katika Umoja wa Afrika na katika duru za kimataifa.

“Tunapinga kauli hii kwa kuwa Tanzania tumekuwa mstari wa mbele kuwasaidia kupata uhuru wa Sahara Magharibi chini ya chama cha ukombozi cha Polisalio,” alisema Shaibu.

Akizungumza hivi karibuni, Waziri Mahiga, alisema Polisalio ni chama cha ukombozi kilichopewa hadhi ya Serikali na uanachama wa Umoja wa Afrika tangu 1982, lakini suala hilo limeanza kuleta utata kisheria.

Baada Ya Diamond, Lynn Ahamishia Majeshi Yake Kwa Chris Brown

Video vixen Irene Hillary maarufu kama Lynn aliyejizolea umaarufu Kupitia video ya Rayvanny ya wimbo wa ‘Kwetu’ amefunguka kuhusu mahaba mazito kwa supastaa wa kimataifa

Lynn alipata umaarufu baada ya kudaiwa kutoka kimapenzi na staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz hadi kubeba mimba yake.

Lakini hivi sasa Lynn ameweka wazi kuwa mapenzi yake yote yamehamia kwa staa wa Muziki kutoka Marekani Chris Brown na kusema Staa Huyo anamkosesha usingizi akimuwaza.

Kwenye mahojiano na Risasi Jumamosi, Lynn alisema kuwa ametokea kumpenda sana mwanamuziki huyo kiasi ambacho haelewi atafanyaje ila anaomba katika maisha yake siku moja akutane naye, amueleze hisia zake.

“Hivi ulishawahi kumpenda mtu mpaka ukawa huelewi sababu? Sasa ndio mimi nilivyo kwa Chris, naamini siku nitaonana naye na kama ikitokea hivyo kwa kweli nitamfikishia hisia zangu, kama atakubali au kukataa, niwe tu nimemuambia, naamini nitakuwa na amani”.

Korea Kaskazini Yasisitiza Ipo Tayari Kwa Mazungumzo na Marekani

Ni nia ya kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un kuwa mkutano kati yake na Rais wa Marekani Donald Trump uendelee, imeeleza taarifa ya vyombo vya habari vya Korea Kaskazini.

Hii ni kutokana na mkutano wa kushtukiza wa siku ya Jumamosi kati ya Kim na Rais wa Korea Kusini, Moon Jae-in.

Rais Trump alisitisha mkutano uliopangwa kufanyika tarehe 12 mwezi Juni kuzungumzia mpango wa nuklia wa Korea Kaskazini, lakini alisema Jumamosi kuwa mambo yanaendelea vizuri sana

Wakati huo huo ujumbe wa Marekani uliripotiwa kwenda Korea Kaskazini siku ya Jumapili.

Balozi wa zamani wa Marekani nchini Korea Kusini, Sung Kim, atafanya mazungumzo na naibu waziri wa mambo ya nje wa Korea Kaskazini kuhusu maandalizi ya mkutano, vyombo vya habari vya Marekani na Korea Kusini vimeeleza.

Mkutano huo ni matunda ya jitihada za kidiplomasia ambazo zilianza mwaka huu kujaribu kuondoa hali ya msuguano uliohofiwa kugeuka kuwa makabiliano ya kijeshi kati ya Korea Kaskazini, Korea Kusini, na Marekani.
Credit:BBC

Mwanafunzi Chuo cha SAUT Ajinyonga Baada ya Timu Yake ya Liverpol Kufungwa

Mwanafunzi wa mwaka wa pili Chuo kikuu cha ‘St. Augustine’ kampasi ya Mbeya Moses Mashaka amejinyonga mara baadaya timu yake ya Liverpol kushindwa kutwaa ubingwa wa klabu bingwa barani ulaya.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Kamanda wa Polisi Jijini Mbeya Naibu Kamishna wa Polisi Mussa Taib amesema Moses (24) amejinyonga mara baadaya ‘kubet’ na timu yake kushindwa kutwaa ubingwa.

“Mwanafunzi wa chuo kikuu cha sauti mwaka wa pili anachukua shahada ya ualimu amefariki baada ya ‘kubet’ pesa ambazo hazijulikani ni kiasi gani na baadaya Liverpol kushindwa ndipo akachukua uamuzi huo”,amesema kamanda Taibu.

Aidha Kamanda Taibu amewataka wanafunzi kuacha kutumia fedha za wazazi kwa mambo yasiyohusiana na masuala mazima ya elimu, kwani matokeo yake ni hasara kwa wazazi.

Sunday, May 27, 2018

Lema alipongeza Bunge, akomaa na Stahiki za Tundu Lissu

Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema amefunguka kuwa bado wanaendelea kutafakari suala la Mbunge wa Sigida Mashariki Tundu Lissu kuhangaika na kutafuta misaada ya matibabu kwa watu mbalimbali duniani, kwani Bunge bado linatafakari kuhusu stahiki zake, haki na gharama za matibabu.

Mhe. Lema amezungumzia hayo ikiwa ni siku moja tangu kutokea kwa kifo cha Mbunge wa Buyungu, Kasuku Bilago aliyefariki wakati akipatiawa matibabu katika hospitali ya Taifa, Muhimbili.

Lema amesema "Mwili wa Marehemu Mhe. Bilago umepata heshima, haki na stahiki ya Kibunge, tumefanya kikao tena Kati ya Bunge, Chama na Familia, wema wa Bunge kwa mwili wa marehemu umekuwa ni wa kifani".

Ameongeza "Wakati tunalishukuru Bunge kwa wema huu, bado tunaendelea kulitafakari la rafiki yetu Lissu aliyeko Ubeligiji".

Lissu ambaye anatibiwa nchini Ubelgiji alipigwa risasi na watu wasiojulikana Septemba 9, 2017 maeneo ya Area D akiwa anatokea katika majukumu yake ya kikazi bungeni Dodoma.

Sababu za Lissu kutotibiwa na Bunge ziliwekwa wazi na Spika wa Bunge, Job Ndugai  siku moja baada ya tukio hilo ambapo alisema kuwa utaratibu wa matibabu kwa mbunge ulikuwa umeshafuatwa lakini familia pamoja na chama  waliamua kumpeleka Nairobi, na siyo kama wao walishindwa kumpeleka nchini India.
Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema amefunguka kuwa bado wanaendelea kutafakari suala la Mbunge wa Sigida Mashariki Tundu Lissu kuhangaika na kutafuta misaada ya matibabu kwa watu mbalimbali duniani, kwani Bunge bado linatafakari kuhusu stahiki zake, haki na gharama za matibabu. Mhe. Lema amezungumzia hayo ikiwa ni siku moja tangu kutokea kwa kifo cha Mbunge wa Buyungu, Kasuku Bilago aliyefariki wakati akipatiawa matibabu katika hospitali ya Taifa, Muhimbili. Lema amesema "Mwili wa Marehemu Mhe. Bilago umepata heshima, haki na stahiki ya Kibunge, tumefanya kikao tena Kati ya Bunge, Chama na Familia, wema wa Bunge kwa mwili wa marehemu umekuwa ni wa kifani". Ameongeza "Wakati tunalishukuru Bunge kwa wema huu, bado tunaendelea kulitafakari la rafiki yetu Lissu aliyeko Ubeligiji". Lissu ambaye anatibiwa nchini Ubelgiji alipigwa risasi na watu wasiojulikana Septemba 9, 2017 maeneo ya Area D akiwa anatokea katika majukumu yake ya kikazi bungeni Dodoma. Sababu za Lissu kutotibiwa na Bunge ziliwekwa wazi na Spika wa Bunge, Job Ndugai siku moja baada ya tukio hilo ambapo alisema kuwa utaratibu wa matibabu kwa mbunge ulikuwa umeshafuatwa lakini familia pamoja na chama waliamua kumpeleka Nairobi, na siyo kama wao walishindwa kumpeleka nchini India.

Mtanzania Aibuka Kidedea Mashindano Ya Kuhifadhi Quran Afrika.....Waziri Mkuu amtaka Sheikh Kishki akaonane na Waziri wa Ardhi atoe maamuzi ya kiwanja

KIJANA wa Kitanzania, Shujaa Suleiman Shujaa ameibuka kidedea na kitita cha sh. milioni 15 katika mashindano ya 19 ya Afrika ya kuhifadhi Quran kwenye kundi la washiriki wa juzuu 30.

Shujaa mwenye miaka 23 ambaye ni mkazi wa Morogoro, amejishindia pia laptop, kiwanja chenye hati eneo la Kigamboni kilichotolewa na kampuni ya Property International ya jijini Dar es Salaam pamoja na dola za Marekani 500 kutoka kwa Bw. Ahmed Seif “Magari” aliyetoa dola 500 kwa washindi wote watano.

Akizungumza na maelfu ya waumini na Watanzania waliofurika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam jana  mchana (Jumapili, Mei 27, 2018), Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewataka Watanzania waendelee kuilinda amani iliyopo nchini kwani ikipotea hakuna atakayeweza kufanya ibada.

“Mtakubaliana nami kuwa amani ya nchi yetu, ndiyo inatufanya tutembee vifua mbele dhidi ya wenzetu, ni neema kubwa ambayo kila muumini anapaswa kuilinda kwani ikipotea hata mkusanyiko wetu huu wa leo si rahisi kufanyika mahali kama hapa,” alisema.

“Leo hii tuko hapa uwanjani kwa sababu tuna amani, kama Serikali isingekuwa inashirikisha Watanzania wote kulinda amani, basi tusingeweza kukutanika hapa. Kuna nchi 18 ziko hapa, na watu wake wamekuja hapa uwanjani kwa kuwa wana uhakika na amani tuliyonayo sisi Watanzania,” alisema.

Alisema katika nchi ambazo amani imetoweka, watu wanalazimika kufanya shughuli za ibada majumbani au kwa kujificha. 
“Wenzetu hao, hawapati fursa adhimu kama hii ya kujumuika pamoja na majirani, ndugu, jamaa na marafiki kusikiliza na kufurahia kisomo cha Quran au kufanya shughuli nyingine za kiuchumi na kijamii,” aliongeza.

Aliwataka Watanzania waendelee kubeza na kupuuza kauli za walio wachache ambao kwao kuzungumzia amani ni kujipendekeza kwa Serikali. “Watu hao wamesahau kwamba tofauti katika Uislamu hazikuanza leo, lakini tofauti hizo hazikuwa sababu ya wema waliotangulia kuacha kuheshimiana na kushirikiana,” alisisitiza.

Mshindi wa pili kwenye kundi hilo la juzuu 30 ni Ahmed Noor wa Sudan ambaye ameshinda sh. 12,564,750 pamoja na laptop akifuatiwa na Muzamil Awadh Mohamed wa Sudan alijishindia sh. milion 7.5 pamoja na laptop zilizotolewa na kampuni ya Camara Education.

Mshindi wa nne ni Abdulally A. Mohammed wa Kenya aliyepata zawadi ya sh. 5,711,000 na wa tano ni Ibrahim Maazur kutoka Niger, aliyepata sh. 3,426,000. Washindi hao wote watano walipewa zawadi ya kwenda hijja na Waziri wa Mambo ya Dini wa Saudi Arabia, Dk. Saleh Ally Sheikh.

Washiriki wengine kwenye kundi la juzuu 30 walitoka nchi za Rwanda, Burundi, Msumbiji Djibouti, Kenya, Ethiopia, Congo DRC, Nigeria, Ghana na Afrika Kusini.

Washiriki wengine waliopewa zawadi ni wale walioweza kuhifadhi Juzuu tatu (washindi watatu), Juzuu tano (washindi watatu); Juzuu 10 (washindi watatu) na Juzuu 20 (washindi watatu).

Viongozi wengine waliohudhuria mashindano hayo ni Makamu wa Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Dk. Mohammed Gharib Billal, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa Tanzania kutoka Saudi Arabia, Comoro, Oman, Uturuki, Kenya, Msumbiji na Nigeria, Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir bin Ally na Rais wa taasisi ya Al-Hikma, Sheikh Sharif Abdilkadir Al-Ahdal.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amemtaka Sheikh Nurdin Mohammed Ahmad (maarufu kama Sheikh Kishki) akaonane na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Bw. William Lukuvi ili atoe maamuzi ya kiwanja chao kilichopo eneo la Matumbi ambacho mwaka jana aliagiza kifuatiliwe taratibu zake na kisha wapatiwe.

“Kuhusiana na suala la kiwanja mlichosema, mamlaka ya awali ni Manispaa ya Temeke na ilishakamilisha taratibu zote za kisheria, ikapeleka kwa Afisa Ardhi wa Mkoa kuona kama limepita kwenye vikao vyote ndipo wanaenda wizarani kupata kibali. Hakuna sababu ya wizara kuikatalia manispaa huku eneo lenyewe likiwa kwenye ramani kuu ya manispaa yenyewe, nenda mumuone Waziri mwenye dhamana, awape ardhi,” alisema.

Waziri Mkuu amefikia hatua hiyo baada ya kupewa taarifa akiwa jukwaani kwamba taasisi ya Al-Hikma iliwasiliana na Manispaa ya Temeke, hadi mkoani wakapewa barua zinaonyesha eneo liko sawa lakini walipofika wizarani wamekwamishwa na Afisa mmoja aliyemtaja kwa jina moja la Mama Mpetula.

Juni 11, mwaka jana katika mashindanio ya 18, taasisi ya Al-Hikma waliomba wapatiwe kiwanja na.118 kwenye kitalu E kilichoshikamana na kiwanja na. 117 chenye shule yao ya Al-Hikma Girls iliyoko Temeke ili waweze kujenga zahanati.

PICHA: Rais Magufuli Alivyokutana na Kufanya Mazungumzo na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 27 Mei, 2018 amekutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa CCM Ndg. Abdulrahman Kinana, Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Katika mazungumzo hayo Mhe. Rais Magufuli alipokea salamu kutoka kwa viongozi wa chama na Serikali wa Afrika Kusini na Zimbabwe ambako hivi karibuni Ndg. Kinana aliongoza ujumbe wa viongozi wa CCM kutembelea nchi hizo na kukutana na viongozi wakuu wa vyama tawala vya ANC na ZANU-PF vinavyoongoza Serikali.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli na Ndg. Kinana wamezungumzia maandalizi ya vikao vya Kamati Kuu ya CCM (CC) na Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC) vitakavyofanyika  tarehe 28-29, Mei, 2018 Jijini Dar es Salaam.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya May 28

TANGAZA HAPA KWA BEI NAFUU