test

Monday, May 28, 2018

Korea Kaskazini Yasisitiza Ipo Tayari Kwa Mazungumzo na Marekani

Ni nia ya kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un kuwa mkutano kati yake na Rais wa Marekani Donald Trump uendelee, imeeleza taarifa ya vyombo vya habari vya Korea Kaskazini.

Hii ni kutokana na mkutano wa kushtukiza wa siku ya Jumamosi kati ya Kim na Rais wa Korea Kusini, Moon Jae-in.

Rais Trump alisitisha mkutano uliopangwa kufanyika tarehe 12 mwezi Juni kuzungumzia mpango wa nuklia wa Korea Kaskazini, lakini alisema Jumamosi kuwa mambo yanaendelea vizuri sana

Wakati huo huo ujumbe wa Marekani uliripotiwa kwenda Korea Kaskazini siku ya Jumapili.

Balozi wa zamani wa Marekani nchini Korea Kusini, Sung Kim, atafanya mazungumzo na naibu waziri wa mambo ya nje wa Korea Kaskazini kuhusu maandalizi ya mkutano, vyombo vya habari vya Marekani na Korea Kusini vimeeleza.

Mkutano huo ni matunda ya jitihada za kidiplomasia ambazo zilianza mwaka huu kujaribu kuondoa hali ya msuguano uliohofiwa kugeuka kuwa makabiliano ya kijeshi kati ya Korea Kaskazini, Korea Kusini, na Marekani.
Credit:BBC

0 comments:

Post a Comment

TANGAZA HAPA KWA BEI NAFUU