test
Showing posts with label AFYA. Show all posts
Showing posts with label AFYA. Show all posts

Monday, July 11, 2016

Wauguzi Manesi Waliosababisha Mama Mjamzito Akajifungulia Korido Watumbuliwa



SHINYANGA: Wauguzi wawili wa kituo cha Afya Lyabukande, wamesimamishwa kazi sababu ya uzembe uliosababisha mwanamke mjamzito kujifungulia kwenye korido.

Pia wamefunguliwa mashtaka kwa tuhuma za kukiuka maadili ya utumishi. ..

Sunday, July 10, 2016

Wasimamishwa kazi baada ya mama kujifungua kwenye korido


Siku chache baada ya vyombo vya habari  kuripoti mjamzito kujifungulia kwenye korido ya Kituo cha Afya Lyabukande, Shinyanga kwa kukosa huduma, uongozi wa Halmashauri ya Shinyanga umewasimamisha kazi watumishi wawili wa kituo hicho kwa tuhuma za uzembe. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Kiomoni Kibamba ambaye kwa sasa ameteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza, jana aliwataja waliosimamishwa kuwa ni pamoja na muuguzi msaidizi wa kituo hicho, Zulfa Mussa na mhudumu katika maabara, Peter Mazengo. 
Kibamba alisema wamewasimamisha kazi na kufunguliwa mashtaka ya kukiuka maadili ya utumishi huku wakipewa siku 14 kujibu kwa utaratibu wa ajira ya utumishi. 
“Baada ya hapo tunasubiri baraza la madiwani ndilo litatoa uamuzi juu yao.” 
Alisema wakati tukio hilo linatokea, watumishi hao walikuwa zamu na kushindwa kumsaidia mjamzito huyo na kitendo hicho kilibainika kuwa cha makusudi na uzembe wa wazi. 
“Awamu hii ya tano ni awamu nyepesi kwa kufanya kazi sababu imenyooka na iko wazi. Mtu anayeona hawezi kwenda na kasi atupishe ili wabaki wanaoweza kutekeleza majukumu yao kwa kufuata kanuni, taratibu na sheria za nchi na nilishasema mara kwa mara suala hili,” alisema Kibamba. 
Kamati iliyoteuliwa kuchunguza jambo hilo, ikiongozwa na Mganga Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Dk Athuman Pembe ilibaini kuwa baada ya mjamzito huyo kujifungua kwenye korido, watumishi ambao hawakuwapo bali walipata taarifa na kufika kumhudumia mtoto ambaye ana afya nzuri na baada ya muda aliruhusiwa kurudi nyumbani. 
Ilivyotokea 
Tukio la mjamzito huo, Margareth Charles (22), mkazi wa Kijiji cha Kizungungu lilitokea Julai 2 baada ya kuelezwa na mtaalamu wa maabara kuwa hakuna huduma waende sehemu nyingine, lakini mama huyo alishindwa kutokana na uchungu.
Mtendaji wa Kata ya Lyabukande, Julius Lugende alisema wananchi wamekuwa wakikilalamikia kituo hicho kwa muda mrefu na ilifikia wakati waliandamana kuwakataa watumishi waliopo kutokana na wajawazito kunyanyasika na kujifungua bila usaidizi.

HIZI NDIZO SABABU 10 ZA KIAFYA ZITAKAZO KUFANYA ULE MAEMBE KILA SIKU,SOMA HAPA NIKUJUZE

Nani  hapendi maembe jamani maembe yanaweza kuitwa mfalme wa matunda yote kwa sababu yana virutubisho
vingi sana vitakavyokusaidia kiafya.Kupunguza uzito,kuongeza kinga ya mwili wako,na mambo mengi ya
urembo kwa wakina dada na wakina kaka pia,kuna sababu lukuki zitakazo kufanya ule maembe kila siku

CHATI ZA KIAFYA KWA ASILIMIA
105 ZA  KALORI
76 ZA VITAMINI C
25 ZA VITAMINI A
11 ZA VITAMINI B6 NA VITAMINI B NYINGINEZO
9 NYUZINYUZI
9 SHABA
7 POTASIAMU
4 MAGNESIAMU

FAIDA ZA KULA EMBE KILA SIKU NI HIZI

1.KUONGEZA UWEZO WA KUONA
 Hii ni kwa sababu ina vitamini A za kutosha kukusasidia katika macho yako

2.INATIBU UGONJWA WA ANAEMIA

3.INASAIDIA KUKUKINGA NA KANSA

4. MAEMBE YANASAIDIA KUPUNGUZA UZITO

5.YANAONGEZA NGUVU ZA MENO NA FIZI

6.YANASAIDIA KUPUNGUKA MAFUTA KWA KIASI KIKUBWA

7.YANASAIDIA KUSAGA KWA CHAKULA

8.YANASAFISHA NGOZI YA USO KWA KIASI KIZURI SANA KWA KUPAKA KATIKA NGOZI YAKO KWA DAKIKA 15
  NA KUOSHA KWA MAJI SAFI
9.INAONGEZA KINGA YA MWILI
TANGAZA HAPA KWA BEI NAFUU