test

Monday, May 21, 2018

Watakaohujumu Miundombinu Tanesco Kukiona

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amewataka Watanzania kuilinda na kuitunza miundombinu ya Shirika la Umeme nchini (Tanesco), huku akiagiza mamlaka husika kuwashughulikia watakaojihusisha na uharibifu wa miundombinu hiyo.

Majaliwa ameyasema hayo jana Mei 21, alipokuwa akizindua uunganishaji wa gridi ya taifa kwa Mkoa wa Lindi na Mtwara iliyofanyika katika Kituo cha kupozea umeme cha Maumbika mkoani hapa.

“Wapo baadhi ya watu wasio na nia njema na serikali wanaharibu miundombinu kwa kung’oa vyuma na kuuza kama vyuma chakavu, hawa ni wahujumu uchumi.

“Naagiza mamlaka zinazohusika kufanya ukaguzi kila eneo linalouza au kununua chuma chakavu kubaini kama kuna miundombinu ya Tanesco na endapo mtaikuta wahusika wawajibishwe kwa mujibu wa sheria,” alisema Majaliwa.

Pamoja na mambo mengine, Waziri Majaliwa amesema kuwa mkakati uliopo sasa ni kuboresha miundombinu ya zamani na kujenga miradi mipya ya umeme ili kuzalisha umeme wa kutosha ili kuwafikia wananchi wengi.

0 comments:

Post a Comment

TANGAZA HAPA KWA BEI NAFUU