test

Monday, May 21, 2018

Ndugai aitaka Serikali kuhakiki mikataba yake na wawekezaji

Spika wa Bunge Job Ndugai ameitaka Serikali kuhakiki mikataba yake na wawekezaji badala ya kusubiri kuwaadhibu wanaohusika na mikataba mibovu.

Akifungua semina ya Chama cha Wabunge walio katika mapambano dhidi ya rushwa (APNAC) bungeni jana Mei 21, Ndugai alisema wabunge wanafahamu namna ambavyo mikataba ilivyoigharimu nchi.

“Eneo hili la mikataba hasa kwa kampuni za nje ya nchi katika madini, nishati za gesi, umeme imekuwa mibovu sana.  Tumeliwa sana katika mikataba hii,” alisema.

Alitaka eneo hilo kuangaliwa kwa umakini ili kuwa na mikataba safi.

“Lazima tuhakikishe tumeziba mianya yote. Sasa hivi inaaminika kuwa rushwa imepungua sana, japo kuna wengine wanasema imebadili sura na imekuwa rushwa kubwa zaidi ya zile za zamani. Sasa hatujui lipi ni kweli inabidi tulifanyie kazi.

“Tusije tukaenda likizo tukidhani imepungua ama imeisha kumbe bado iko huko iliko. Bunge linapambana sana na masuala ya rushwa kupitia kamati zote za Bunge lakini zinazoshika bendera ni zile za usimamizi,” alisema.

Awali akimkaribisha Spika Ndugai, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika alisema inaonyesha kuwa rushwa inapungua nchini.

0 comments:

Post a Comment

TANGAZA HAPA KWA BEI NAFUU