Mwenyekiti wa Baraza la vijana Chadema (BAVICHA), Patrick Ole Sosopi,
amesema amewahi kushawishiwa na wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM)
ili aweze kuhamia chama hicho tawala.
Ole Sosopi amesema hayo leo Mei 16 akiwa studio za EATV katika kipindi
cha KIKAANGONI kinachorushwa kila siku ya Jumatano kuanzia saa 8:00
mchana hadi saa 10:00 za jioni na kuongeza kuwa yeye hana thamani ambayo
itaweza kumnunua kwakuwa ni tegemeo la vijana wa CHADEMA nchi nzima.
“Ndiyo nimewahi kushawishiwa na kiukweli ukiwa bora watataka kukuonesha
kwamba utakua bora zaidi, kumbe sio sahihi, ubora wa Ole Sosopi
unaoonekana leo CHADEMA, kama ningekuwepo CCM inawezekana ninsingepata
hata ubalozi wa nyumba kumi, naamini kule hawathamini uwezo bali ni nani
anakujua na historia yako” amesema Ole Sosopi.
Kiongozi huyo wa BAVICHA Taifa ameongeza kuwa watu hao walikua
wakimshawishi kwa kutumia njia ya kiurafiki kwa kumwambia kuwa kutokana
na ubora wake alistahili awepo upande wa Chama cha Mapinduzi (CCM).
Novemba 21, 2017 aliyekuwa mwenyekiti wa Baraza la Vijana Chadema
(BAVICHA) Patrobasi Katambi alitangaza kuhamia Chama cha Mapinduzi (CCM)
kwa madai ya kufurahishwa na utendaji kazi wa mwenyekiti wa chama hicho
Rais Dkt. John Magufuli
Thursday, May 17, 2018
Nimeshawishiwa Kuhamia CCM- Mwenyekiti wa BAVICHA
Related Posts:
Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Manunuzi Wasomwa ..Waliohukumiwa kwa Rushwa Kunyimwa Zabuni, Mikataba yote Kuwa na Mashuhuda MUSWADA wa Marekebisho ya Sheria ya Manunuzi wa Mwaka 2016, umesomwa kwa mara ya kwanza bungeni jana na kuwekwa wazi kwa umma, na moja ya vifungu vinavyopendekezwa ni kuzuia mtu yeyote aliyewahi kuhukumiwa k… Read More
SOMA:Shirikisho La Wanafuzi Vyuo Vya Elimu Ya Juu Tanzania Lalaani Kauli Za Gwajima Juu Ya Viongozi Wa CCM Siku chache baada ya Kiongozi wa Kanisa la Ufufuo na Uzima Josephat Gwajima kuwashutumu viongozi wa CCM kwamba wanamipango ya kutomkadhi chama Rais Dk. John Magufuli, Shirikiho la Wanafunzi wa vyuo vya Elimu ya Juu Tan… Read More
Rais Magufuli Amteua Dk Rubaratuka Kuwa Mwenyekiti Mpya wa Bodi ya Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) Rais John Magufuli amemteua Prof. Ignas Aloys Rubaratuka kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) katika kipindi cha miaka mitatu kuanzia Mwezi Aprili mwaka huu. Taarifa hiyo ilitolewa na Dk. L… Read More
Polisi Wamuwinda Askofu Gwajima Kwa Masaa 7 Bila Mafanikio........Ni Baada ya Kusambaa kwa Video Akimsema Vibaya Rais Mstaafu Jakaya Kikwete Polisi jana walipiga kambi kwa saa saba kwenye geti la nyumba ya Askofu Josephat Gwajima wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, wakitaka kumkamata bila ya mafanikio. Polisi hao walikuwa kama wageni wa askofu huyo wakisubiri… Read More
Serikali Mbioni Kufungua Ubalozi mpya Qatar TANZANIA inatarajia kufungua ubalozi wake nchini Qatar kwa lengo la kuendeleza na kuimarisha zaidi uhusiano na ushirikiano kati ya nchi hizo huku ikitilia mkazo katika sekta za gesi asilia, utalii, usafiri wa anga na … Read More
TANGAZA HAPA KWA BEI NAFUU
0 comments:
Post a Comment