Mwenyekiti wa Baraza la vijana Chadema (BAVICHA), Patrick Ole Sosopi,
amesema amewahi kushawishiwa na wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM)
ili aweze kuhamia chama hicho tawala.
Ole Sosopi amesema hayo leo Mei 16 akiwa studio za EATV katika kipindi
cha KIKAANGONI kinachorushwa kila siku ya Jumatano kuanzia saa 8:00
mchana hadi saa 10:00 za jioni na kuongeza kuwa yeye hana thamani ambayo
itaweza kumnunua kwakuwa ni tegemeo la vijana wa CHADEMA nchi nzima.
“Ndiyo nimewahi kushawishiwa na kiukweli ukiwa bora watataka kukuonesha
kwamba utakua bora zaidi, kumbe sio sahihi, ubora wa Ole Sosopi
unaoonekana leo CHADEMA, kama ningekuwepo CCM inawezekana ninsingepata
hata ubalozi wa nyumba kumi, naamini kule hawathamini uwezo bali ni nani
anakujua na historia yako” amesema Ole Sosopi.
Kiongozi huyo wa BAVICHA Taifa ameongeza kuwa watu hao walikua
wakimshawishi kwa kutumia njia ya kiurafiki kwa kumwambia kuwa kutokana
na ubora wake alistahili awepo upande wa Chama cha Mapinduzi (CCM).
Novemba 21, 2017 aliyekuwa mwenyekiti wa Baraza la Vijana Chadema
(BAVICHA) Patrobasi Katambi alitangaza kuhamia Chama cha Mapinduzi (CCM)
kwa madai ya kufurahishwa na utendaji kazi wa mwenyekiti wa chama hicho
Rais Dkt. John Magufuli
Thursday, May 17, 2018
Nimeshawishiwa Kuhamia CCM- Mwenyekiti wa BAVICHA
Related Posts:
Waziri Mkuu Majaliwa Akagua Kiwanda Cha Kutengeneza Vigae Cha Goodwill Ceramic Cha Mkuranga WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali itahakikisha viwanda vinajengwa kwa wingi nchini kwani ndiyo msingi imara wa ukuaji wa uchumi na muarobaini wa tatizo la ajira hususan kwa vijana. “Mbali na kukuza uchumi… Read More
Rais Magufuli Afufua Safai ya Kuhamia Dodoma Kwa Kuwapeleka Mashujaa Dodoma RAIS John Magufuli ameonesha nia ya kuhamia Dodoma kwa kuanza kushughulikia masuala muhimu, ikiwamo ya kuzindua awamu ya kwanza ya upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Dodoma na kuhamishia maadhimisho ya Siku ya Mashujaa mko… Read More
Pingamizi la Tundu Lissu Kutaka Afutiwe Kesi ya Uchochezi Lagonga Mwamba MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam imetupilia mbali maombi ya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema) ya kufutiwa mashitaka ya uchochezi yanayomkabili na wenzake watatu. Hakimu Mkazi Mkuu, E… Read More
Picha ya Rais Zuma wa Afrika Kusini akimbusu msichana huyu yawa gumzo Picha ya msichana akimbusu Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma imezua utata nchini humo. Picha hizo zilisambaa Jumatano hii baada ya msichana huyo kuziweka kwenye mitandao ya kijamii. “We will check the matter,” alisema… Read More
Picha 5 za Mbunge wa Kigoma mjini Zitto Kabwe Alivyofunga ndoa jana Zanzibar Mbunge wa Kigoma mjini, Zitto Kabwe jana aliuacha rasmi ukapera baada ya kufunga ndoa na mpenzi wake aliyemvisha pete ya uchumba miezi miwili iliyopita, ndoa na tafrija zote zilifanyika Zanzibar. … Read More
TANGAZA HAPA KWA BEI NAFUU
0 comments:
Post a Comment