test

Friday, May 11, 2018

Jiji la Mwanza kukosa umeme hadi saa Kumi na Moja Jioni

Maeneo ya katikati ya Jiji la Mwanza leo Mei 11, 2018 yatakosa umeme kwa saa nane baada ya transfoma na nyaya za umeme kuanguka eneo la Kauma na kuziba barabara ya stesheni.

Kwa mujibu wa taarifa ya  Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) zinaeleza kuwa nishati hiyo itarejea kuanzia saa 11 jioni.

Ofisa uhusiano wa Tanesco jijini Mwanza, Flaviana Moshi amesema nguzo hizo zimedondoka saa 2 asubuhi na kuathiri upatikanaji wa umeme kwa maeneo mengi ya jiji hilo.

0 comments:

Post a Comment

TANGAZA HAPA KWA BEI NAFUU