test

Saturday, May 26, 2018

Kamanda Mambosasa Azungumzia 'Mabilioni ya Dr Shika'

Kamanda wa polisi kanda maalum ya Dar es salaam Lazaro Mambosasa amesema swala la Dk. shika kuingiza pesa zake Tanzania hana uhakika nalo na mtu kutumiwa hela kihalali si kosa 
Amesema kuwa kama taarifa hizo ni za uongo anaweza kupuuzwa ila endapo kauli yake italeta madhara basi hatua zitachukuliwa.

Mambosasa amezungumza hayo leo pindi alipokuwa anaongea na waandishi wa habari akitoa ripoti za jeshi la polisi kuwashikilia watuhumiwa mbambali kwa kufanya makosa ya unyang’anyi kwa kutumia silaha za moto.

”Mtu kutumiwa hela kama ni halali haziingii kwenye pesa ambazo zinatakatishwa au hela ambazo zinapatikana kwa njia isiyo halali si kosa lakini kama ni muongo tu anajisema basi kuna mawili anaweza kupuuzwa lakini kama kauli zake zitamwaathiri yeyote anaweza kuja kulalamika na jeshi la polisi likachukua hatua” amesema Mambosasa.

Mambosasa amezungumza hayo pindi alipokuwa anajibu swali la mmoja wa waandishi wa habari baada ya kuhoji juu ya uhalali wa pesa za Dk. Luis Shika ambaye hivi karibuni taarifa zimeeleza tayari ameingiza mabilioni yake ya fedha nchini Tanzania.

Siku chache zilizopita Dkt. Louis Shika alivieleza baadhi ya vyombo vya habari nchini juu ya ujio wa fedha zake na baadhi ya vipande vya dhahabu zilizokuwa nje ya nchi kuwa tayari zimewasili nchini kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere (JKNIA) na kupelekwa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) kwa ajili ya kuhakikiwa.

Taarifa hizo zilizua mjadala mkubwa mtandaoni ambapo watu walionesha kutokuamini kwa ujio huo wa pesa za  Dk. Shika wakidhani ni stori zisizo na ukweli ndani yake.

Hata hivyo Shika alithibitisha ujio wa mali hizo na kuonyesha baadhi ya nyaraka zinazothibitisha umiliki wa mali hizo.

Mo Salah atacheza World Cup? Daktari wa timu atoa neno hili.

Mtanange wa yule Bingwa wa Ulaya umekamilika. Real Madrid wameshinda taji lao la tatu mfululizo kwa ushindi wa mabao matatu kwa moja. Golikipa wa Liverpool Karius akisababisha uzembe ulioigharimu timu hao baada ya kurusha mpira kimakosa na ukagomga Benzema aliyegfunga bao la kwanza kabla ya Mane kusawazisha. unga magoli mawili. Bale alitokea benchi na kufunga mabao mawili.

Niliwahi kusema kinyago cha Gazzaniga (Kombe la Dunia) kiliwanyima mastaa wengi usingizi. Majeraha ilikuwa changamoto kubwa sana kwa wachezaji wa pande zote.
kilichotokea leo ni kitu ambacho wengi tulitarajia kutapoteza ladha ya mchezo huu.

Mo Salah ambaye alikuwa mchezaji tegemezi wa Liverpool hivi leo atolewa kwenye mchezo mapema kabisa baada ya kuumia bega. Ilikuwa ni kashkash kati yake yeye na Sergio Ramos. Ramos alikwenda kumkaba Salah na ilionekana wakishikana mkono. Picha na video zinaonesha kuwa alimvuta mkono na kumsababisha Salah kuondoka vibaya na kulalia bega lake.

Je wachambuzi wakubwa wanasemaje?
Rio Ferdinand
Ramos amekaba vyema. Alifanya kitu ambacho mlinzi yeyote angefanya. Sidhani kama alidhamiria.
Frank Lampard
mnapokuwa mmesogeleana sana mara nyingi ni rahisi sana kushikana mikono. ile ni bahati mbaya sana.

Rio na Lampard hawa ni waingereza na wana haki ya kutoa Maoni yao. Jana nilimsikia David Beckham aliweka pembeni sana suala la Uzalendo. Na aliweka mapenzi yake dhahiri kuwa Real inafaa iifunge Liverpool. Rio nae ni hasimu mkubwa wa Liverpool. Bila shaka ukiangalia ile video utagundua hakuna ajali. kuna tofauti kubwa ya kushikana na kumvuta mtu kwa makusudi ukidhamiria.

John Simpson anasema hivi
Nimeangalia maoni ya wachambuzi wakubwa, wanasema lile tukio ni ajali. Sawa. Lakini ukimwangalia Ramos wakati Salah anatolewa nje utagundua alidhamiria.

kuna baadhi ya video zinamuonesha Ramos akitabasamu na Mwamuzi wa pembeni.
David Maddock anasema
Inauma sana. Ramos amefanya kitendo cha kikatili haswa. Hajaharibu tu ndoto za Salah za Uefa pia huenda ameharibu ndoto wa Wamisiri wote.

Mo Salah taarifa zinasema mishipa ya bega imeachana. Na majibu kamili yatatolewa wakirudi jijini Liverpool. Hii inaleta wasiwasi mkubwa kama atahitaji kufanyiwa upasuaji. na itamlazimu kukosa michuano ya kombe la dunia.

hata hivyo taarifa za hivi punde zinasema kuwa ukurasa wa timu ya taifa ya Misri umeweka taarifa kuwa Mo Salah atacheza michuano ya kombe la dunia

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya May 27


Thursday, May 24, 2018

Mwanamke Amuua Mumewe kwa Kisu...Ni Baada ya Kugoma Kumpikia Chakula Kisha Ugomvi Ukaibuka

Sophia  Salehe, mkazi wa Kata ya Namiongo, Newala mkoani Mtwara, anashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani humo, kwa tuhuma za kumuua mume wake kwa kumchoma kwa kisu.

Mauaji hayo yalitokana na ugomvi baina ya mtuhumiwa ambaye inadaiwa kuwa alikataa wito wa mumewe kupika chakula baada ya kutokushiba.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, Lucas Mkondya, amesema tukio hilo lilitokea juzi mkoani humo.

Kwa mujibu wa Mkondya, mwanamume huyo alikufa papo hapo baada ya kuchomwa kisu na mke wake.

Alisema siku ya tukio majira ya saa 1:30 usiku, mwanamke huyo alimwandalia mume wake chakula na kumpatia.

“Kile chakula kilikuwa kidogo, mume wake, Ahmed Salim, alimtaka arudi jikoni kwa ajili ya kupika tena chakula kwa kuwa hakikumtosha. Hapo ndipo palitokea ugomvi wakalumbana na wakaendelea kugombana na mkewe akachukua kisu na kumchoma kifuani,” alisema Kamanda Mkondya.

Kamanda Mkondya alisema Salim alifariki dunia papo hapo baada ya kutokwa na damu nyingi kwenye jeraha.

Aidha, alisema katika tukio hilo wanamshikilia na mwanaume mmoja ambaye hakutaka jina lake liandikwe kutokana na uchunguzi unaoendelea.

Alisema wanamshikilia kijana huyo kwa kuwa katika tukio hilo alikuwapo, hivyo watakapopata maelezo yatakayojiridhisha kutohusika ataachiwa.

“Bado huyu kijana tunamhoji ni kwa nini hakutoa msaada wa kuamua ugomvi huo. Hapa tunataka kujua na yeye amehusika au la na kwa huyu mwanamke taratibu zikikamilika atafikishwa mahakamani,” alisema.

Aidha, Kamanda alisema mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Newala kwa ajili ya kusubiri taratibu za mazishi.

Sugu Ampongeza Mwandosya kwa Kumtembelea Gerezani

Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi, maarufu Sugu (Chadema), ameliambia Bunge kuwa wakati akiwa gerezani, alipokea salamu kutoka kwa viongozi na wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) huku akimpongeza Prof. Mark Mwandosya kwa kuwa mwana CCM pekee aliyekwenda kumsalimia gerezani.

Akichangia bungeni jijini Dodoma jana mjadala wa makadirio ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa mwaka ujao wa fedha, Sugu aliwapongeza viongozi na wabunge wa CCM kwa kumtumia salamu gerezani huku akidai wengi wao waliogopa kwenda kumjulia hali.

Hata hivyo, Sugu alisema CCM waliwakilishwa vizuri na waziri wa zamani Prof. Mwandosya ambaye ndiye pekee wa chama tawala hicho aliyefika gerezani kumjulia hali.

Mbunge huyo ambaye jana alikuwa wa kwanza kuchangia mjadala huo, pia alitumia fursa hiyo kutoa pole kwa wananchi wa Mbeya ambao alidai waliungana naye kutumikia kifungo hicho.

"Nawashukuru watu wote waliopaza zauti zao kulaani kifungo dhidi yangu," alisema Sugu katika maneno yake ya utangulizi kabla ya kujikita katika hoja iliyokuwa bungeni.

Mbunge huyo mwanzoni mwa mwaka huu alihukumiwa kifungo cha miezi mitano gerezani baada ya kukutwa na hatia kisha kuachiwa wiki mbili zilizopita kwa msamaha wa Rais.

Katika mchango wake jana, Sugu alisema matukio ya uhalifu na vifungo dhidi ya wanasiasa kama yeye yanayotokea nchini yanawafanya baadhi ya wawekezaji kuogopa kuja kuwekeza nchini.

Alisema pamoja na kwamba Tanzania inaweza kuwa na jitihada za kuwashawishi wawekezaji kutoka nje kuwekeza nchini, mkakati huo huenda usifanikiwe kwa kuwa wawekezaji wanapenda kuwekeza katika nchi zenye usalama kuliko nchi zenye vurugu na mauaji.

Sugu pia alimshauri Rais aanze kusafiri kwenda nje ya nchi akisisitiza kuwa safari za nje zina faida kama ilivyokuwa enzi za uongozi wa Rais mstaafu Jakaya Kikwete aliyekuwa akisafiri mara kwa mara.

“Pamoja na hayo, serikali haiwatendei haki Watanzania wanaoacha kazi nje na kuja kufanya kazi nchini kwa sababu inataka iwalipe mishahara midogo kama ilivyotokea kwa bosi mmoja wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC)," Sugu alisema.

Musukuma amkana Bashe Sakata la Kutekwa na Usalama wa Taifa

Mbunge wa Geita Vijijini, Joseph Musukuma Kasheku, amefungukia madai yaliyowahi kutolewa na Mbunge wa Nzega Mjini Hussein Bashe, kwamba walitekwa na watu wa usalama wa Taifa ni ya uongo na kwamba kilichotokea walikamatwa na askari na mbinu zilizotumika ni zile wanazofundishwa bungeni.

Musukuma ametoa kauli hiyo jana  wakati alipokuwa anazungumza kwenye kipindi cha Kikaangoni kinachorushwa na  EATV , ambapo alifafanua kwamba walikuwa wakidhaniwa kufanya uhalifu.

Musukuma alisema kwamba "Mara ya kwanza kulala polisi nimelala nikiwa mwana- CCM, mara ya kwanza Dodoma, mara ya pili ni Geita, na nilikubali kwa sababu wala hatukutekwa, nilikuwa na kina Bashe, nilimsikia rafiki yangu Hussein Bashe alisema tumetekwa, hatukutekwa".

"Tulikamatwa tukapelekwa polisi, tukapekuliwa, tulipoonekana hatuna hatia tukaachiwa , hatukutekwa. Sikumjibu Hussein Bashe aliposema tumetekwa kwa sababu sikuwepo, nasema hapa hatukutekwa," Musukuma.

Aprili 11, 2017 Mbunge wa Nzega Mjini(CCM) Hussein Bashe aliwataka wabunge kuacha unafiki kuhusu Usalama kuwateka watu na kwamba yeye ni mmoja wa watu waliokamatwa wakati wa mkutano Mkuu wa CCM.

"Mimi nimekamatwa na kuteswa na Usalama wa Taifa. Nimenyanyaswa sana nchi hii. Ikibidi mnifukuze CCM - " alisema Bashe wakati Waziri wa Tamisemi,(kabla hajaenguliwa katika nafasi hiyo) George Simbachawene kumtaka Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe kuthibitisha kuwa matukio ya ukamataji yanafanywa na usalama wa Taifa.

Babu Tale Apelekwa mahabusu kwa muda usiojulikana

Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imemwamuru mkurugenzi wa kampuni ya Tiptop Connections Company Limited, Hamis Shaban Taletale maarufu kwa jina la Babu Tale, kukaa mahabusu katika kituo cha Polisi akisubiri amri ya kupelekwa kifungoni.

Mahakama hiyo katika uamuzi uliotolewa na Naibu Msajili, Wilbard Mashauri Februari 16, iliamuru Babu Tale na ndugu yake Idd Shaban Taletale wakamatwe na kupelekwa kifungoni baada ya kushindwa kutekeleza hukumu yake.

Hukumu hiyo iliyotolewa na Jaji Agustine Shangwa Februari 18, 2016, iliwaamuru ndugu hao kumlipa fidia ya Sh250 milioni, Mhadhiri wa Dini ya Kiislamu, Sheikh Hashim Mbonde kwa makosa ya kutumia mahubiri yake kibiashara bila ridhaa yake.

Kutokana na amri hiyo ya kuwakamata, Babu Tale alitiwa mbaroni juzi na jana alipelekwa mahakamani hapo kwa ajili ya amri ya kumpeleka kifungoni, lakini alilazimika kurudishwa mahabusu Kituo Kikuu cha Polisi kwa kuwa Naibu Msajili aliyetoa amri ya kuwakamata hakuwepo.

Amri hiyo ya kumrejesha rumande ilitolewa na naibu msajili wa mahakama hiyo, Ruth Massam hadi hapo Naibu Msajili Mashauri aliyetoa amri ya kuwafunga atakaporejea kutoka Dodoma alikokwenda kikazi.

Kwa kuwa haijulikani ni lini atarejea, Babu Tale ambaye pia ni meneja wa msanii maarufu wa muziki wa kizazi kipya, Abdul Nassib maarufu kama Diamond Platnum, atalazimika kukaa mahabusu kwa muda usiojulikana mpaka atakaporejea.

Hati ya kuwakamata Babu Tale na ndugu yake ilitolewa April 4, mwaka huu kutokana na maombi ya Sheikh Mbonde kupitia wakili wake Mwesigwa Muhingo.

Sheikh Mbonde aliwasilisha maombi hayo baada ya Babu Tale na nduguye kushindwa kutekeleza hukumu hiyo, yaani kumlipa kiasi hicho walichoamriwa na Mahakama wala kubainisha mali za kampuni yao, au zao binafsi, ili zipigwe mnada kulipia fidia hiyo.

Katika kesi ya msingi, Sheikh Mbonde aliieleza Mahakama kuwa Juni 6, 2013 aliingia makubaliano na kampuni hiyo ili irekodi mawaidha yake na kuziuza kisha wagawane faida, lakini baada ya kurekodi masomo saba, walimwambia kuwa walikuwa wameachana na mpango huo.

Alieleza kuwa baadaye alibaini kuwa mikanda ya video ya mfumo wa DVD zenye mawaidha yake zilikuwa zikiuzwa katika mikoa mbalimbali huku zikiwa na majina na namba za simu za wakurugenzi wa kampuni hiyo, ndipo akafungua kesi hiyo.

Baada ya Sheikh Mbonde kuwasilisha maombi ya kuwafunga jela Babu Tale na nduguye, mahakama ilimwelekeza Sheikh Mbonde kuwalipia wafungwa hao watarajiwa pesa za chakula mahakamani na kumtaka pesa kwa ajili ya matumizi mengine kuziwasilisha gerezani.

Kwa mujibu wa Mahakama, gharama za kuwahudumia wafungwa hao wakiwa gerezani ni kama ifuatavyo:

Vifaa ambavyo ni taulo ya kuogea Sh12,000; godoro Sh40,000; mto wa kulalia Sh10,000; chandarua Sh13,000; mashuka manne Sh48,000; kandambili (malapa) Sh3000; mswaki na dawa ya meno Sh2,000 ambazo jumla ni Sh128,000 kwa mtu mmoja na kwa watu wote wawili ni Sh256,000.

Chakula, kifungua kinywa Sh7,000; chakula cha mchana Sh8,000; maji lita tatu 3,000, jumla Sh18,000 kwa mtu mmoja kwa siku na kwa wote wawili ni Sh36,000. Wote kwa mwezi ni Sh1,080,000.

Pia, kuna fedha za tahadhari kiasi cha Sh800,000 kwa kila mfungwa na kwa wote wawili jumla ni Sh1,600,000.

Sheikh Mbonde alisema kuwa tayari ameshawalipia wafungwa hao fedha za chakula ya mwezi mmoja kiasi cha Sh1,080,000 na kusema ataendelea kuwalipia kiasi kama hicho kila mwezi.

Alisema fedha za matumizi mengine kama yalivyoainishwa na mahakama, ziko tayari na kwamba hizo ataziwasilisha kwa uongozi wa gereza baada ya wafungwa hao kufikishwa huko.

Wanawake 40 Kunyongwa Iraq

Serikali inatarajia kuwanyonga wachumba 40 wa wanamgambo wa Dola ya Kiislamu (IS) kulipiza kisasi kwa wapiganaji hao wa jihadi kuikalia kwa miaka mitatu ardhi ya Iraq wakati wa mapigano yaliyosababisha maelfu ya watu kuuawa kikatili.

Wanawake hao ambao ni wa kigeni walikiri mahakamani kwamba na wao ni waathirika wa IS, walipewa dakika 10 kila mmoja kutetea uhai wao kabla ya majaji kufikia uamuzi wapewe adhabu kali.

Wanawake hao walishutumiwa na mahakama ya Iraq na raia wa kawaida kwa kuwapa msaada waume zao wapiganaji waliosababisha maafa katika eneo walilokuwa wanakalia kuanzia mwaka 2014 hadi 2017.

Mwanamke mmoja mwenye uraia wa Ufaransa aitwaye Djamila Boutoutao, 29, alidai kuwa alidhani alikuwa anaolewa na mwanamuziki wa miondoko ya rap.

“Ni baada ya kuwasili Uturuki kwa ajili ya ‘mapumziko’ ya wiki moja ndipo nilipogundua ya kuwa mume wangu ni mpiganaji wa kijihadi,” alisema Djamila.

“Mimi ni mwathirika. Mume wangu alinipiga na kunifungia kwenye pango na watoto wangu nilipokataa kumfuata (hadi Iraq).’

Djamila ni mmoja wa raia wa Ufaransa wapatao 1,900 na wasafiri wa kigeni wanaokadiriwa kuwa 40,000 waliosafiri hadi Syria na Iraq kujiunga na miliki ya khalifa.

Katika hukumu yake ya hivi karibuni, ambako aliomba asitenganishwe na binti yake, Djamila aliwaambia waandishi wa habari wa gazeti la The Guardian: “Nachanganyikiwa hapa. Nakabiliwa na adhabu ya kifo au kifungo cha jela maisha. Hakuna anayeniambia chochote, si balozi wetu wala watu ndani ya gereza.”

“Jamani nawasihi msiwaache waondoke na binti yangu. Niko tayari kuwapa fedha endapo mtawasiliana na wazazi wangu. Tafadhali niokoeni.”

Takriban wanawake 40 ndio wamehukumiwa kifo na watu wengine 300 wenye mafungamano na IS wameshauawa.

Wednesday, May 23, 2018

Msukuma: Kuna Baadhi ya Wizara Zinatia Kichefuchefu na Kila Nikiwaona Mawaziri Wake Natamani Kukimbia

Mbunge wa Geita Vijijini Mh. Joseph Musukuma amesema baadhi ya Wizara ni kichefuchefu na kuna Waziri hata akifumba macho akifumbua akamuona anakimbia kutokana na anavyofanya kazi zake katika Wizara anayoongoza ndio maana baadhi wamepata taabu kupitisha Bajeti zao Bungeni.

Akiongea jana Mei 23, kwenye kipindi cha Kikaangoni cha EATV , Musukuma aliwataja baadhi ya Mawaziri wanaozitendea haki Wizara zao kuwa ni Waziri William Lukuvi wa Ardhi na Ummy Mwalimu wa Afya.

''Unajua sio kila Wizara unachangia tu zingine zimekamilika hata Mawaziri wake waliposimama kusoma Bajeti zao ili zipitishwe hakuna aliyepinga, lakini kuna Waziri hata ukinifumba macho nikifumbua tu nikamuona nakimbia'', amesema.

Musukuma alisema baadhi ya Mawaziri wamekuwa wakifanya kazi kwa mihemuko ndio maana wao kama wabunge wanajitahidi kuwashauri wanapokuwa wameenda tofauti.

Aidha ameeleza kuwa kitendo cha Wabunge kushauri vitu kadhaa Bungeni hawamaanishi lazima wasipitishe bajei ila wanachofanya ni kushauri kisha kupitisha ili serikali ikafanyie kazi ushauri wao.

Msukuma: Wanaolisema Vibaya Jeshi la Polisi Wanakosea....Siku Likiacha Kazi Watu Watabakana bila Kutongozana

Mbunge wa Geita Vijijini Joseph Musukuma, amesema kwamba watu wanaomsema Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda kuhusu watu wasiojulikana na wanao likashifu jeshi la polisi na kulituhumu kwa mambo yasiyofaa wanalikosea jeshi hilo, kwani bila wao tusingekuwa salama.

Musukuma ameyasema hayo jana alipokuwa akiongea na East Africa Television, na kusema kwamba iwapo jeshi la polisi likiacha kazi kufanya kazi hata kwa siku moja hakutakuwa na amani, kwani watu watafikia hatua ya kubakana bila kutongozana.

“Ilitengenezwa tu chuki kuwa watu wasiojulikana wanatumwa na Makonda, sijui na nani!! Mara polisi, hii dhana si nzuri, haya matukio yametokea sehemu nyingi, Kibiti huko, sijui wapi huko, ila mnalichafua tu jeshi la polisi , Siku jeshi la Polisi likisema liache kufanya kazi, hali itakuwa mbaya, hatutatongozana tutabakana.”, alisema Musukuma.

Sambamba na hilo Musukuma amesema watu wanaofanya hivyo hawako sahihi, kwani badala yake wanapaswa kulishukuru jeshi hilo kwa jukumu la kuwalinda wao na mali zao.

Facebook Yaendelea Kuomba Msamaha

Mkurugenzi wa Facebook Mark Zuckerberg ameomba msamaha kwenye Bunge la Ulaya kutokana na madhara yaliyosababishwa na kuvuja kwa data za watumiaji wa mtandao huo na pia kwa kushindwa kupambana na habari za uongo/ feki.

Mkurugenzi Mtendaji wa Facebook Mark Zuckerberg aliomba msamaha kwa watumiaji wa Ulaya wa mitandao ya kijamii na kuahidi kupambana na habari feki za uongo  na vile vile ameahidi kwamba data za watumiaji hao zitalindwa vyema.

Zuckerberg alifika mbele ya viongozi wa makundi ya kisiasa wa Bunge la Ulaya baada ya Facebook kukubali kwamba ilitoa taarifa binafsi za watumiaji wapatao milioni 87 kwa kampuni ya Cambridge Analytica ya nchini Uingereza, zikiwemo zile za watumiaji karibu milioni 2.7 kutoka kwenye nchi za Umoja wa Ulaya. Facebook ilikubali kwamba ilitoa taarifa hizo binafsi kwa njia isiyo sawa.

Hata hivyo Zuckerberg aliyakwepa baadhi ya maswali magumu aliyoulizwa na wabunge hao, na kisha kuomba msamaha kutokana na sera za Facebook zilizorahisisha kuenea kwa habari feki wakati wa uchaguzi wa rais wa Marekani wa 2016 na pia katika matokeo ya kura ya maoni juu ya Uingereza kujiondoa kutoka Umoja wa Ulaya.

Baadhi ya wabunge wa Umoja wa Ulaya hata hivyo wamelalamika kwamba Zuckerberg hakutoa majibu halisi juu ya matumizi mabaya ya data za mamilioni ya watumiaji wa mtandao huo. 
Jan Philipp Albrecht, mjumbe maalum wa Umoja wa Ulaya anayeshughulikia ulinzi wa data za Umoja huo (GDPR) amesema ipo haja ya kuwepo ulinzi mkubwa.

Mjumbe huyo maalum anayeshughulikia masuala ya ulinzi wa data katika Umoja wa Ulaya amesema pia uangalizi unahitajika zaidi kwenye shughuli za mtandao huo wa Facebook, kwa mfano katika kuitenganisha Facebook na WhatsApp au Facebook Messenger ambapo hatua kama hiyo sasa itakuwa ni chaguo la mtu binafsi . Bwana Albrecht amesema hilo ni moja kati ya maswali ambapo Mark Zuckerberg hakutoa majibu ya kina.

Zuckerberg ameomba msamaha kwa niaba ya kampuni yake kwa kushindwa kuzuia kutumiwa vibaya baadhi ya mifumo yake ya internet huku wengi wa wabunge waliokuwepo katika mahojiano hayo wakisema bilionea huyo wa Facebook alishindwa kutoa majibu yaliyoweza kuwatoa wasiwasi walio nao.

Mfumo wa kujibu maswali ulimruhusu Zuckerberg kujibu maswali hayo mwishoni, na hivyo kuwaacha wabunge wakiwa wamekata tamaa kutokana kushindwa kupata majibu ya moja kwa moja kwa maswali yao.

Rais wa Bunge la Ulaya Antonio Tajani alimwambia Zuckerberg kwamba kufika kwake kumetoa ishara muhimu ya heshima  yake kwa Bunge hilo pamoja na wananchi wa Ulaya.

Iran yaendelea kupinga masharti ya Marekani

Iran imeendelea kupinga masharti kutoka Marekani ya kufanyia mabadiliko sera yake ya kigeni na mpango wake wa nyuklia huku mshirika wake Syria, ikitupilia mbali wito wa Marekani kuviondoa vikosi vya Iran nchini humo.

Ufaransa, mmoja ya mataifa yenye nguvu barani Ulaya, iliosikitishwa na hatua ya Marekani kujiondoa katika mkataba wa nyuklia uliyotiwa saini mwaka 2015, imesema hatua ya Marekani ya kuiongezea vikwazo zaidi Iran, itawaimarisha zaidi wanasiasa wenye msimamo mkali nchini Iran.

Jumatatu wiki hii waziri wa mambo ya nchi za nje wa Marekani Mike Pompeo aliitishia iran kuwa itakabiliwa na vikwazo zaidi katika historia iwapo haitaachana na ushawishi wake wa kikanda, akiishutumu nchi hiyo kuunga mkono makundi ya silaha katika mataifa kama vile Syria Lebanon na Yemen.

Pompeo aliyasema haya wiki mbili baada ya rais Trump kujiondoa katika mpango wa kimataifa wa nyuklia wa Iran, uliopelekea taifa hilo kuondolewa vikwazo kufuatia hatua yake ya kukubali kusitisha uendelezaji wa mpango huo. 
Mataifa yenye nguvu barani Ulaya yanauona mkataba huo kama nafasi nzuri ya kuizuwia Iran kutengeneza silaha za nyuklia.

Kwa upande wake Waziri wa Mambo ya nchi za nje wa Iran Mohammad Javad Zarif amesema Pompeo amerejelea shutuma za zamani dhidi ya nchi yake ila safari hii shutuma hizo zimetolewa kwa ukali zaidi.

Naye afisa wa ngazi ya juu wa jeshi la Iran Meja jenerali Mohammad Bagheri, amesema Iran haitaisujudia Marekani katika shinikizo lake la kudhibiti shughuli zake za kijeshi. 
Mjini Paris, Waziri wa Mambo ya nchi za nje wa Ufaransa Jean-Yves Le Drian amesema hatua ya Marekani kujiondoa katika mkataba huo wa nyuklia na kuiwekea Iran vikwazo itazidisha misimamo mikali na kuhatarisha eneo hilo.

Le Drian amesema Ufaransa itaendelea kutekeleza makubaliano ya mkataba huo hata kama inakubaliana na Marekani kwamba shughuli za nyuklia za Iran pamoja na makombora  zinapaswa kudhibitiwa.

Huku hayo yakiarifiwa Syria imetupilia mbali wito wa Marekani wa kuviondoa vikosi vya Iran nchini humo. Katika vita vya Syria vilivyodumu miaka 7, Iran imekuwa ikitoa msaada muhimu kwa  jeshi la serikali ya Bashar al Assad.

Waziri Mkuu: Tanzania Inahitaji Wawekezaji ili Kupata fursa ya mitaji na teknolojia za kisasa

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Tanzania bado inahitaji wawekezaji na kupitia kwenye uwekezaji, inapata fursa ya mitaji na teknolojia za kisasa.

Ametoa kauli hiyo jana (Jumatano, Mei 23, 2018) wakati akizungumza na Balozi wa Tanzania nchini Canada, Bw. Alfayo Kidata ambaye alifika kumuaga kwenye makazi yake jijini Dar es Salaam.

Waziri Mkuu amemtaka Balozi Kidata atumie fursa ya uwepo wake nchini Canada kuangalia namna ya kuisadia nchi kuimarisha sekta za kilimo, madini na utalii.

“Tukiimarisha sekta hizi, uchumi ndani ya nchi unakua lakini pia tunategemea kutumia nchi rafiki kukuza uchumi wetu wa ndani kwa maana ya kukuza mitaji na kupata teknolojia za kisasa,” amesema.

“Ukienda huko mkakati wako mkubwa uwe ni kuzingatia mpango wa Taifa wa maendeleo wa miaka mitano lakini zaidi mkakati wetu wa kukuza uchumi wa viwanda,” amesisitiza.

Amemtaka Balozi huyo akasimamie pia suala la upatikanaji wa masoko kwa ajili ya mazao yanayozalishwa nchini ili wafanyabiashara na wakulima wa Tanzania waweze kuuza bidhaa zao nje ya nchi.

“Hapa nyumbani tuna mazao matano ambayo tumeazimia kuyafufua lakini masoko ya ndani hayatoshi, kwa hiyo kazi yako mojawapo ukiwa huko ni kututafutia masoko,” amesema.

Waziri Mkuu amemweleza Balozi Kidata azingatie pia suala zima la kuongeza idadi ya watalii. “Tunataka ukasaidie kutangaza nchi yetu ili watalii waje kuona vivutio vyetu. Tunataka kuongeza idadi ya watalii kutoka milioni mbili ya sasa hadi kufikia milioni tano ifikapo mwaka 2020,” amesema.

Alimtaka Balozi huyo akafuatiilie pia fursa za masomo kwa ajili ya Watanzania wanaotaka kusoma Canada na Cuba. 

“Nilipoongea na Makamu wa Rais wa Cuba, aliahidi kuongeza idadi ya Watanzania wanaotaka kusomea udaktari. Kwa hiyo, ukifika itabidi ufuatilie ahadi hiyo,” ameongeza.

Waziri Mkuu pia alimsisitizia Balozi Kidata akifika huko awatambue na kuwaunganisha Watanzania waishio Canada na awahamasishe wafanye kazi ili waweze kuwekeza nyumbani.

Kwa upande wake, akizungumza baada ya kuagana na Waziri Mkuu, Balozi Kidata alisema atahakikisha anayafanyia kazi maelekezo yote aliyopewa na Waziri Mkuu.

Alisema anatambua kwamba Canada ina idadi ya watu zaidi ya milioni 40 na atafanya juhudi zaidi za kuitangaza Tanzania ili waje kuona vivutio vilivyopo nchini. Pia atafuatilia fursa za mafunzo kwa wanafunzi wa Kitanzania.

“Kwenye suala la uchumi wa viwanda, tunahitaji kuwa na uzalishaji wa mazao ya kutosha. Kwa hiyo tunahitaji kuwana kilimo cha uhakika na cha muda wote kuliko. Tunahitaji kupata utaalamu na mitaji kwa ajili ya mashamba ya umwagiliaji,” alisema.

Alisema kuwepo kwa kilimo cha umwagiliaji, kutasaidia kuwe na uhakika wa upatikanaji wa malighafi zitazakotumika kwenye viwanda.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

Kiwanda Cha Nyama Chapigwa Faini Ya Milion 5 Dodoma Kwa Kushindwa Kukidhi Vigezo Vya Usafi Wa Mazingira


Labels
Kiwanda cha nyama cha Tanzania (TMC) kimepigwa faini ya Milion 5 baada ya kukiuka kanuni za uhifadhi wa mazingira na kuchelewa kutekeleza agizo walilopewa kuhakikisha wanafanyiakazi maagizo waliyopewa juu ya kufanyiakazi kanuni za utunzaji wa mazingira ikiwemo kufanya tathmini mazingira kabla ya kuanza kazi.

Akizungumza wakati akikagua machinjio hayo na kiwanda hicho cha nyama Naibu waziri wa nchi Ofisi ya makamu wa Rais Muungano na Mazingira Kangi Lugola  Ameelezea kutoridhishwa na hali ya mazingira kiwandani hapo.

Akitoa tamko hilo ,Naibu waziri Lugola alisema kuwa kulingana na sheria za usimamizi na usafi wa mazingira ni sharti kiwanda hicho kitozwe faini ili iwe fundisho kwa viwanda vingine kufuata taratibu ikiwa ni pamoja na kufanya tathmini ya mazingira kabla ya kuanza shughuli za uzalishaji.

Pamoja na mambo mengine  Lugola alikiagiza kiwanda hicho kuelekeza taka ngumu kwenye dampo la jiji lililopo Chidaya -Ntyuka ili kuepuka madampo yasiyo rasmi yanayozagaa katikati ya jiji na kukuta mizoga ya nyama ikiwa imezagaa maeneo mbali mbali.

Awali akisoma taarifa kwa naibu waziri Lugola,Mtendaji  Mkuu wa kiwanda hicho Aron Luziga alizungumzia changamoto zilizopo  kiwandani hapo kuwa ni pamoja na mfumo wa maji taka usio rasmi kutokana na gharama kubwa ya ujenzi pamoja na upatikanaji wa umeme wa uhakika hali inayokwamisha shughuli za uzalishaji .

Alisema,hali ya kukatika katika kwa umeme kiwandani hapo inakwamisha shughuli za uzalishaji hivyo kuiomba serikali kuangalia namna ya kuboresha miundombinu ya umeme ili kukidhi mahitaji .

"Lengo la kiwanda hiki ni kuwa kinara katika uzalishaji wa nyama na kusafirisha nchi nyingi zaidi duniani hii ikiwa ni pamoja na uchakataji wenye kiwango kuendana na soko La kimataifa," alisema Luziga.

Wakati huo huo  Naibu waziri  Kangi Lugola  ameliagiza Baraza la usimamizi wa mazingira la Taifa (NEMC) kushirikiana na uongozi wa jiji la Dodoma kukagua kwa undani mifumo ya maji taka ya kiwanda cha kukamua mafuta ya alizeti cha Sunshine kilichopo katika kijiji cha Zuzu.

Hatua hiyo imekuja kutokana na kushindwa kuibaini mifumo ya majitaka kiwandani hapo kutokana na kuwa kiwanda kimesitisha uzalishaji kutokana uhaba wa malighafi kiwandani hapo.

Kutokana na hayo Naibu waziri Lugola emeutaka uongozi wa kiwanda hicho kuingia mkataba na wakulima ili waweze kupata malighafi ambazo zitawezesha kiwanda hicho  kuwa na uzalishaji wakati wote.

"Ni kweli tunahitaji Tanzania ya viwanda,lakini viwanda hivyo  vije kwa kuzingatia sheria za mazingira ili kuyahifadhi na kwa manufaa ya vizazi vijavyo," alisema.

Hata hivyo alisema viwanda vinapaswa kuchochea wananchi kuondokana na umaskini hivyo ni wajibu kushirikiana na wananchi bega kwa bega kupata solo la uhakika.

Lukuvi, Mengi Wakutana Kujadili Fursa za Uwekezaji

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi amekutana na Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Dkt. Reginald Mengi ili kuzungumza na kutambua fursa zinazopatikana za uwekezaji katika sekta ya Ardhi nchini.

Dkt. Mengi amekutana jana na Mhe. Lukuvi ofisini kwake kanda ya Dar es salaam ambapo walijadili mambo mbalimbali ambayo Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imeyafanya katika sekta ya ardhi  na kutoa fursa  kwa wawekezaji wa ndani kuwekeza kwa urahisi.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya May 24


TANGAZA HAPA KWA BEI NAFUU